30 September 2017


MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Omar Khamis Othman amesema, katika kutekeleza agizo la rais wa Zanzibar Dk: Ali Mohame Shein kuhusiana na walimu watoro, ameanza kwa kupata orodha ya walimu wote wa mkoa wake, ili iwe rahisi wakati atakapofanya ziara za ghafla skulini, kuwatambua.

Akizungumza na Zanzibarleo Ofisini kwake Wete alisema, watahakikisha maagizo yote yaliyotolewa na Rais wanayatekeleza ipasavyo likiwemo hilo la waalimu watoro.

Alisema kuwa, walimu hao atawafuatilia kwa kuwapitia katika skuli zao wanazosomesha bila ya kutoa taarifa, ili kuweza kuwabaini walimu wenye kufanya tabia ya utoro.

“Tutakwenda skuli zote kimya kimya na tukifika tu tunazichukua simu za za walimu waliopo, ili wasije wakawapigia”, alisema Mkuu huyo.

Mkuu huyo alieleza kuwa, watazifuatilia skuli moja baada ya moja na endapo watabaini kuna walimu wenye tabia hiyo, hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

“Ikiwa mwalimu ana matatizo basi tupate taarifa yake kamili, lakini kinyume na hivyo tutamchukulia hatua za kisheria”, alieleza.

Aidha alieleza kuwa, pia watahakikisha wanapeleka miundombinu ya maji maskulini, ili kuondosha tatizo hilo lililopo kwa baadhi ya skuli, kwani yote yamo katika mkakati wa kufanyia kazi.

Akizungumzia agizo jengine kwa soko la Tumbe Wilaya ya Micheweni Pemba, Mkuu huyo alisema, soko hilo lipo kwenye matengenezo, ambapo ndani ya miezi miwili litaweza kutumika.

“Sasa hivi wanasubiri huduma ya maji safi na salama, ili waingie ndani ya soko, hivyo tutahakikisha ndani ya miezi miwili wafanyabiashara wetu wataingia ndani ya soko hilo”, alisema Mkuu huyo.


Hayo ni miongoni mwa maagizo aliyoyatoa Raisi wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein katika mkoa huo ili yatekelezwe, ambapo tayari maagizo yote yamo katika mkakati wa kufanyia kazi.

About Me:

My Name is Hussein H. Hussein, I am a Journalist by proffessional, dealing with Radio and TV Braodcastin, News Gathering and Writting, Creating Radio and TV adverts, Producing Radio and TV programs, Events Coverage, Editing Visual and Audio Contents, Shooting, Photography, Graphic designing and Social Media Contents


Connect With Me: TWITTER | FACEBOOK | GOOGLE PLUS