30 September 2017


WANANACHI kisiwani Pemba, wamepongeza hutuba ya rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Mhe: Dk Ali Mohamed Shein, alioitoa kwenye kilele cha maadhimisho ya sherehe za elimu bila ya malipo, yaliofanyika hivi karibuni kisiwani humo.

Walisema hutuba  hiyo ni miongoni mwa hutuba kadhaa zinazotolewa na rais huyo na kuibua hisia, mawazo mapya ndani ya jamii, jambo ambalo huwazidisha upendo kwa kiongozi wao.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, baadhi ya wananchi hao walisema, hutuba hiyo ilikuwa imejaa kila aina ua tendaji, utekelezaji, ahadi na mafanikio yaliopo ndani ya serikali anayoiongoza.

Mmoja katia ya wazazi hayo, Abdull-hamid Juma Makame wa Mchanga mdogo wilaya ya Wete, alisema yeye kwenye hutuba hiyo, lililomvutia ni pale rais alipotangaaza kufuta michango ya elimu ya sekondari.

Alisema tamko hilo kwake, limempa hisia mpya kwamba rais huyo amekuwa akiwajali wanyonge wa nchi hii, kwa lengo la kuona watoto wote, wanapata elimu bila ya kujali uwezo wa wazazi na walezi wao”,alifafanua.

Nae Mashavu Himid Mbaruok wa Wingwi mapofu wilaya ya Micheweni, alisema mara zote rais huyo wa Zanzibar anapotoa hutuba kwenye sherehe mbali mbali za kitaifa, hulenga kuwapatia wananchi huduma sawa.

“Mimi sikutarajia kuwa, kwa vile ameshafuta michango ya elimu ya msingi mwaka jana, na atangaaze kufuta michango ya sekondari, lakini amefanifaya na mimi kama mazazi mwenye watoto wanne mwakani wanaoingia sekondari napongeza”,alifafanua.

Hata hivyo Muhidini Ameir Ali wa Machomane  Chakechake, alisema hutuba hiyo ya rais alioitoa Septemba 23, inafaa kuandikiwa kitabu chake maalum, ili ihifadhiwe na ije isomwe na vizazi vijavyo.

Alisema hutuba hiyo ya raisi, ilieleza historia ya kielimu Zanzibar kabla na baada ya mapinduzi matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964, ambayo skulini haisomeshwi.

“Mimi kwenye hutuba hile ya rais, nililoliona kwangu ni kubwa na inafaa kuwekewa kumbu kumbu, ni suala la historia ya elimu, na sasa ndani ya awamu hii ya saba ilivyoimarishwa”,alieleza.

Kwa upande wake Habiba Mjaka Kombo wa Mtambile, alisema kilichomvutia yeye kwenye hutuba ya rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Mhe: Dk Ali Mohamed Shein, ni ahadi ya kujenga skuli tisa za ghorofa Unguja na Pemba.

Aidha alisema jengine lililomvutia ni kuona jinsi rais alivyotekeleza upanuzi wa skuli 23 na nyengine kufanyiwa matengenezo makubwa, ununuzi wa vifaa vya maabara na  samani.

Mwenyekiti wa masheha wilaya ya Micheweni Dawa Juma Mashindo, alisema yeye alivutiwa na kila jambo, ingawa rais kutangaaza kipaumbele cha kutanua elimu kilimkosha roho.


Septemba 23, mwaka huu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe: dk Ali Mohamed Shein, alikamilisha kilelele cha maadhimisho ya siku ya elimu bila ya malipo, uwanja wa Gombani kwa hutuba yake, alioeleza mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na kutangaaza kufuta michago ya elimu ya sekondari.

About Me:

My Name is Hussein H. Hussein, I am a Journalist by proffessional, dealing with Radio and TV Braodcastin, News Gathering and Writting, Creating Radio and TV adverts, Producing Radio and TV programs, Events Coverage, Editing Visual and Audio Contents, Shooting, Photography, Graphic designing and Social Media Contents


Connect With Me: TWITTER | FACEBOOK | GOOGLE PLUS