2 October 2017


WASAIDIZI wa sheria wanaoendelea na masomo yao, kwenye Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba, wametakiwa kuyachukua kwa umakini mkubwa mafunzo wanayopewa, ili wapate kuisiadia jamii kwa uhakika na sio kubabaisha.

Kauli hiyo, imetolewa na Mratibu wa Kituo hicho Fatma Khamis Hemed, wakati alipokuwa akifungua mafunzo ya siku mbili, kwa wasaidizi hao wa sheria, juu ya kukumbushwa sheria mbali mbali, ambazo wanapaswa kuielimisha jamii.

Alisema msaidizi wa sheria bora, ni yule anaefanyakazi zake kwa umakini na baada ya kupewa mafunzo ya kisheria kuyasikiliza vyema na kisha kuifundisha jamii yake, na kinyume chake ataendelea kufanya kazi kwa mazoea.

Alisema pamoja na kwamba wasaidizi hao wa sheria wanadarasa yao kila mwisho wa mwezi, juu ya masomo mbali mbali, lakini pia mafunzo kama hayo ya siku mbili, wakiwa makini wataongeza uwelewa wa kazi zao.

“Mafunzo haya ya kuwakumbusha nyinyi sheria mbali mbali kama ya ushahidi na ile ya maendeleo ya karafuu, mkiwa makini mtatoa msaada wa kisheria vyema kwa jamii”,alifafanua.

Katika hatua nyengine Mratibu huyo, aliwataka wasaidizi hao wa sheria, kuendelea kujisomea mambo mbali ya kisheria, ili waongeze ufanisi kwenye kazi yao ya kuihudumia jamii.

Mapema Mratibu wa mafunzo hayo Safia Saleh Sultan, alisema wasaidizi wa sheria, wanalojukumu la kuwasaidia wananchi juu ya mambo kadhaa ya kisheria, hivyo mafunzo na taaluma wanazopewa ndio dira.

Akiwasilisha mada ya haki za wanawake kwa mujibu sheria, alisema wanayohaki ya kupewa elimu, kusikilizwa, ajira na nafasi ya uongozi kama walivyo wanaume.

“Mwanamke anatambulika kisheria kuwa nae anapaswa kupewa haki na fursa sawa na mwanamme, na pia yapo matamko mbali mbali yaliochapuzi hilo, likiwemo la kimataifa la haki za bidamu”,alifafanua.

Mapema wakili wa serikali kutoka Afisi ya Mkurugenzi wa mashitaka kisiwani Pemba, Juma Ali Juma, alisema sheria mpya ya ushahidi no 9 ya mwaka 2016, baada ya kufutwa ile ya mwaka 1917, sasa inatambua ushahidi wa kieletroniki.

Alieleza kuwa, sheria hiyo kwa sasa pia inaukubali ushahidi wa mtoto au mtu mwenye ulemavu wa kutozungumza, jambo ambalo hapo kabla hilo halikukubalika.

“Jamii lazima muielimisha kuwa, sheria mpya ya ushahidi, sasa imeimarishwa suala la ushahidi , hivyo wasiwe na mashaka iwapo kuna mtoto kabakwa na hakuna mtu mwengine alieshuhudia”,alifafanua.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, walisema bado jamii inahitaji elimu kwa upana zaidi, maana kesi nyingi hufutwa na mahakama kutokana na mashahidi kutohudhuria.

Walisema, jamii inadhani kesi zote zinazofutwa mahakamani, hutokana na mahakimu na waendesha mashitaka wamekula rushwa, ambapo wakati mwengine huwa sio sahihi.


Katika mafunzo hayo ya siku moja, mada kadhaa zilijadiliwa, ikiwa ni pamoja na sheria ya kuwalinda wari na watoto wa mazazi mmoja no 4 ya mwaka 2005, sheria ya mtoto no 6 ya mwaka 2011, sheria ya ushahidi no 9 ya mwaka 2016, sheria ya Maendeleo ya karafuu ya mwaka 2014 na kanuni yake.

About Me:

My Name is Hussein H. Hussein, I am a Journalist by proffessional, dealing with Radio and TV Braodcastin, News Gathering and Writting, Creating Radio and TV adverts, Producing Radio and TV programs, Events Coverage, Editing Visual and Audio Contents, Shooting, Photography, Graphic designing and Social Media Contents


Connect With Me: TWITTER | FACEBOOK | GOOGLE PLUS

HABARI ZINGINE
Habari Mpya za Hivi Karibuni
Older Post